Thursday, March 19, 2015

FALSAFA YA FIZIKIA

Falsafa ya fizikia Katika namna nyingi fizikia inaonekana kuwa tawi la falsafa ya kale ya kigiriki . Kuanzia jitihada za mwanzo za Thales kueleza tabia za maada, hadi kwa uthibbitisho wa Democritus kwamba maada lazima ipungue hadi hali ya invariant , astronomia ya kiptolemi ya anga[[fuwele]] na kitabu cha Aristotle fizikia (kitabu cha kale cha fizikia Kilichojaribu kuchambua na kufafanua mwendo kutokana na uoni wa kifalsafa), wanafalsafa mbalimbali walikuza nadharia zao .juu ya asilia. Fizikia ilijulikana kama falsafa ya asili hadi mwishoni mwa karne ya 18. Mnamo karne ya 19 ,fizikia ilidhihirika wazi kuwa tapo jingine tofauti na falsafa na sayansi zingine. Fizikia pamoja na sayansi zingine zilizosalia, hutegemea.gov falsafa ya kisayansi kutoa uchambuzi wa kina na wa kutosha wa mbinu za kisayansi. Mbinu za kisayansi zinatumia aina ya ufikiri wa priori na ufikiri wa posteriori na matumizi ya Bayesian inference kupima uhalali wa nadharia husika. Maendeleo ya fizikia yamejibu maswali mengi ya wanafalsafa wa zamani, lakini pia kuibua maswali mapya. Somo la masuala ya kifalsafa inayozunguka fizikia, falsafa ya fizikia, inahusisha masuala kama asili ya nafasi na wakati, determinism, na mtazamo wa kimetafizikia kama empiricism, naturalism na realism. Wanafizikia wengi wameandika kuhusu maana za kifalsafa za kazi zao, katika hilo , Laplace, ambaye aliongoza determinism ya kawaida, na Erwin Schrödinger, ambaye aliandika juu ya kwanta/vifurushi kimakenika. Mwanamahesabu na mfizikia bwana Roger Penrose amekuwa akiitwa ni mwanaplato Stephen Hawking, kwa maoni anayojadili katika kitabu chake cha 'Barabara kuelekea ukweli' (The Road to Reality).Hawking anajichukulia mwenyewe kuwa mredaksheni asiye aibu na anayachukulia mambo kwa maoni ya Penrose.

1 comment: